Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 49:8-14 Biblia Habari Njema (BHN)

8. “Wewe Yuda, ndugu zako watakusifu.Adui zako utawakaba shingo;na ndugu zako watainama mbele yako.

9. “Wewe Yuda, mwanangu, ni kama mwanasimbaambaye amepata mawindo yake akapanda juu.Kama simba hujinyosha na kulala chini;simba mwenye nguvu, nani athubutuye kumwamsha?

10. “Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda,wala bakora ya utawala miguuni pake,mpaka atakapofika yule ambaye ni yake;ambaye mataifa yatamtii.

11. “Atafunga punda wake katika mzabibuna mwanapunda wake kwenye mzabibu bora.Hufua nguo zake katika divai,na mavazi yake katika divai nyekundu.

12. “Macho yake ni mekundu kwa divai,meno yake ni meupe kwa maziwa.

13. “Zebuluni ataishi sehemu za pwani,pwani yake itakuwa mahali pa kuegesha meli.Nchi yake itapakana na Sidoni.

14. “Isakari ni kama punda mwenye nguvu,ajilazaye kati ya mizigo yake.

Kusoma sura kamili Mwanzo 49