7. “Nalaani hasira yao maana ni kali mno,na ghadhabu yao isiyo na huruma.Nitawatawanya katika nchi ya Yakobo,nitawasambaza katika nchi ya Israeli.
8. “Wewe Yuda, ndugu zako watakusifu.Adui zako utawakaba shingo;na ndugu zako watainama mbele yako.
9. “Wewe Yuda, mwanangu, ni kama mwanasimbaambaye amepata mawindo yake akapanda juu.Kama simba hujinyosha na kulala chini;simba mwenye nguvu, nani athubutuye kumwamsha?
10. “Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda,wala bakora ya utawala miguuni pake,mpaka atakapofika yule ambaye ni yake;ambaye mataifa yatamtii.
11. “Atafunga punda wake katika mzabibuna mwanapunda wake kwenye mzabibu bora.Hufua nguo zake katika divai,na mavazi yake katika divai nyekundu.