Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 49:7-11 Biblia Habari Njema (BHN)

7. “Nalaani hasira yao maana ni kali mno,na ghadhabu yao isiyo na huruma.Nitawatawanya katika nchi ya Yakobo,nitawasambaza katika nchi ya Israeli.

8. “Wewe Yuda, ndugu zako watakusifu.Adui zako utawakaba shingo;na ndugu zako watainama mbele yako.

9. “Wewe Yuda, mwanangu, ni kama mwanasimbaambaye amepata mawindo yake akapanda juu.Kama simba hujinyosha na kulala chini;simba mwenye nguvu, nani athubutuye kumwamsha?

10. “Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda,wala bakora ya utawala miguuni pake,mpaka atakapofika yule ambaye ni yake;ambaye mataifa yatamtii.

11. “Atafunga punda wake katika mzabibuna mwanapunda wake kwenye mzabibu bora.Hufua nguo zake katika divai,na mavazi yake katika divai nyekundu.

Kusoma sura kamili Mwanzo 49