Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 49:23-33 Biblia Habari Njema (BHN)

23. “Wapiga mishale walimshambulia vikali,wakamtupia mishale na kumsumbua sana.

24. “Lakini upinde wake bado imara,na mikono yake imepewa nguvu,kwa uwezo wa Mwenye Nguvu wa Yakobo,kwa jina la Mchungaji, Mwamba wa Israeli;

25. “kwa Mungu wa baba yako atakayekusaidia,kwa Mungu mwenye nguvu atakayekubariki;upate baraka za mvua toka juu mbinguni,baraka za maji ya vilindi vilivyo chini,baraka za uzazi wa akina mama na mifugo.

26. Baraka za baba yako zishinde baraka za milima ya milele,ziwe bora kuliko vilima vya kale.Baraka hizo na ziwe juu ya kichwa cha Yosefu,juu ya paji lake yeye aliyekuwa ametengwa na ndugu zake.

27. “Benyamini ni mbwamwitu mkali;asubuhi hula mawindo yake,na jioni hugawa nyara.”

28. Hayo ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hayo ndiyo maneno aliyowaambia baba yao alipowabariki, kila mmoja wao kama alivyostahili.

29. Kisha Israeli akawaagiza wanawe hivi, “Mimi karibu nife na kujiunga na watu wangu. Nizikeni pamoja na wazee wangu katika pango lililoko shambani mwa Efroni Mhiti,

30. kule Makpela, mashariki ya Mamre, nchini Kanaani. Abrahamu alinunua pango na shamba hilo kwa Efroni, Mhiti, liwe lake la kuzikia.

31. Huko ndiko walikozikwa Abrahamu na mkewe Sara; huko ndiko walikozikwa Isaka na mkewe Rebeka; na huko ndiko nilikomzika Lea.

32. Shamba hilo na pango lake lilinunuliwa kwa Wahiti.”

33. Yakobo alipomaliza kuwausia wanawe, aliirudisha miguu yake kitandani, akatoa roho akajiunga na wazee wake.

Kusoma sura kamili Mwanzo 49