Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 49:20-24 Biblia Habari Njema (BHN)

20. “Ardhi ya Asheri itatoa mavuno kwa wingi,naye atatoa chakula kimfaacho mfalme.

21. “Naftali ni kama paa aliye huru,azaaye watoto walio wazuri.

22. “Yosefu ni kama mti uzaao,mti uzaao kando ya chemchemi,matawi yake hutanda ukutani.

23. “Wapiga mishale walimshambulia vikali,wakamtupia mishale na kumsumbua sana.

24. “Lakini upinde wake bado imara,na mikono yake imepewa nguvu,kwa uwezo wa Mwenye Nguvu wa Yakobo,kwa jina la Mchungaji, Mwamba wa Israeli;

Kusoma sura kamili Mwanzo 49