Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 49:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yakobo akawaita wanawe, akasema, “Kusanyikeni pamoja niwaambieni mambo yatakayowapata siku zijazo.

2. “Kusanyikeni msikie, enyi wana wa Yakobo,nisikilizeni mimi Israeli, baba yenu.

3. “Wewe Reubeni ni mzaliwa wangu wa kwanza,nguvu yangu na tunda la ujana wangu.Wewe wawapita ndugu zako kwa ukuu na nguvu.

4. “Wewe ni kama maji ya mafuriko.Lakini hutakuwa wa kwanza tena,maana ulipanda kitandani mwangu mimi baba yako,wewe ulikitia najisi;naam wewe ulikipanda!

5. “Simeoni na Lawi ni ndugu:Silaha zao wanatumia kufanya ukatili,

6. lakini mimi sitashiriki njama zao;ee roho yangu, usishiriki mikutano yao,maana, katika hasira yao, walimuua mtu,kwa utundu wao walikata mshipa wa ng'ombe.

Kusoma sura kamili Mwanzo 49