Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 4:16-22 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Kisha Kaini akaondoka mbele ya Mwenyezi-Mungu, akawa anaishi katika nchi ya Nodi, upande wa mashariki wa Edeni.

17. Kaini akalala na mkewe, naye akapata mimba, akamzaa Henoki. Kaini akajenga mji akauita kwa jina la Henoki mwanawe.

18. Henoki akamzaa Iradi, naye Iradi akamzaa Mehuyaeli; Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, naye Methushaeli akamzaa Lameki.

19. Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada na mwingine Sila.

20. Ada alimzaa Yabali ambaye alikuwa baba yao wafugaji waishio mahemani.

21. Ndugu yake alikuwa Yubali; huyo alikuwa baba yao wanamuziki wote wapigao zeze na filimbi.

22. Sila naye alimzaa Tubal-kaini, ambaye alikuwa mhunzi wa vyombo vyote vya shaba na chuma. Dada yake Tubal-kaini alikuwa Naama.

Kusoma sura kamili Mwanzo 4