Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 39:20-23 Biblia Habari Njema (BHN)

20. akamchukua Yosefu na kumtia gerezani, mahali walipofungwa wahalifu wa mfalme.

21. Lakini hata humo gerezani Mwenyezi-Mungu alikuwa pamoja na Yosefu akimfadhili hata kumfanya apendeke mbele ya mkuu wa gereza.

22. Hivyo mkuu wa gereza alimweka Yosefu awe mkuu wa wafungwa wote humo gerezani; kila kitu kilichofanyika humo kilifanywa kwa mamlaka yake.

23. Huyo mkuu wa gereza hakujishughulisha tena na kitu chochote alichokabidhiwa Yosefu kwa maana Mwenyezi-Mungu alikuwa pamoja na Yosefu na kufanikisha kila kitu alichofanya.

Kusoma sura kamili Mwanzo 39