Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 39:12-20 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Basi, mke wa Potifa alimshika joho lake na kumwambia, “Lala na mimi!” Lakini Yosefu akamwachia vazi lake mikononi mwake, akakimbilia nje.

13. Hapo, yule mwanamke alipoona kwamba Yosefu ameliacha vazi lake mikononi mwake na kukimbilia nje,

14. akawaita watumishi wa nyumbani mwake na kuwaambia, “Tazameni! Huyu Mwebrania tuliyeletewa anatuaibisha. Alikuja kwangu akitaka kunishika kwa nguvu, lakini nikapiga kelele.

15. Aliposikia napiga kelele, aliliacha vazi lake, akakimbilia nje!”

16. Basi, yule mwanamke akaliweka vazi hilo mpaka mumewe aliporudi nyumbani.

17. Akamsimulia kisa kile akisema, “Huyu mtumishi Mwebrania uliyemleta kwetu alinijia ili kuniaibisha.

18. Lakini mara tu nilipopiga kelele, aliliacha vazi lake na kukimbilia nje.”

19. Basi, bwana wake Yosefu alipoyasikia maneno ya mkewe, kwamba ndivyo mtumishi wake alivyomtendea, akawaka hasira,

20. akamchukua Yosefu na kumtia gerezani, mahali walipofungwa wahalifu wa mfalme.

Kusoma sura kamili Mwanzo 39