Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 38:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Wakati huo, Yuda alitengana na ndugu zake, akaenda kukaa na mtu mmoja Mwadulami, jina lake Hira.

2. Akiwa huko, Yuda akamwona binti Shua, Mkanaani, akamwoa.

3. Binti Shua akapata mimba akazaa mtoto wa kiume, Yuda akamwita Eri.

4. Akapata mimba nyingine, akajifungua mtoto wa kiume, akamwita Onani.

5. Kisha akapata mtoto mwingine wa kiume, akamwita Shela. Wakati Shela alipozaliwa, Yuda alikuwa Kezibu.

6. Baadaye Yuda alimwoza mtoto wake wa kwanza Eri, kwa mwanamke aitwaye Tamari.

7. Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu mbele ya Mwenyezi-Mungu; hivyo Mwenyezi-Mungu akamuua.

8. Basi, Yuda akamwambia Onani, “Mchukue mke wa ndugu yako marehemu, kwani ndivyo inavyokupasa kufanya, upate kumzalia nduguyo watoto.”

9. Lakini Onani alijua kwamba hao watoto wasingekuwa wake. Kwa hiyo, alipolala na mke wa nduguye, alimwaga chini mbegu ya uzazi, asije akampatia nduguye watoto.

Kusoma sura kamili Mwanzo 38