Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 37:27-30 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Afadhali tumwuze kwa hawa Waishmaeli, lakini tusiguse maisha yake, kwani yeye ni ndugu yetu; yeye ni damu moja nasi.” Ndugu zake wakakubaliana naye.

28. Wafanyabiashara Wamidiani walipofika mahali hapo, hao ndugu wakamtoa Yosefu katika shimo, wakamwuza kwa Waishmaeli kwa bei ya vipande ishirini vya fedha; nao wakamchukua Yosefu hadi Misri.

29. Basi, Reubeni aliporudi kwenye lile shimo, na asimwone Yosefu tena, akazirarua nguo zake kwa huzuni,

30. akawaendea ndugu zake, akawaambia, “Kijana hayupo nami niende wapi?”

Kusoma sura kamili Mwanzo 37