Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 37:15-23 Biblia Habari Njema (BHN)

15. mtu mmoja akamkuta akitangatanga mbugani, akamwuliza, “Unatafuta nini?”

16. Yosefu akamjibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Tafadhali, niambie mahali wanakochunga wanyama.”

17. Yule mtu akamwambia, “Bila shaka wamekwisha ondoka, kwa sababu niliwasikia wakisema kwamba wanakwenda Dothani.” Basi, Yosefu akawafuata ndugu zake, akawakuta huko Dothani.

18. Ndugu zake walipomwona akiwa mbali na kabla hajafika karibu, wakafanya mpango wa kumuua.

19. Waliambiana, “Tazameni! Yule mwota ndoto anakuja.

20. Haya, tumuue na kumtupa ndani ya shimo mojawapo. Baadaye tutasema kwamba ameuawa na mnyama wa porini. Halafu tutaona hizo ndoto zake zitakuwaje.”

21. Lakini Reubeni aliposikia maneno hayo, akataka kumwokoa mikononi mwao; basi akawaambia ndugu zake, “Tafadhali, tusimuue.

22. Msimwage damu. Ila mtumbukizeni katika shimo hili hapa mbugani, lakini msimdhuru.” Alisema hivyo kusudi aweze kumwokoa Yosefu mikononi mwao, na baadaye amrudishe kwa baba yake.

23. Yosefu alipowafikia ndugu zake, wao wakamvua kanzu yake.

Kusoma sura kamili Mwanzo 37