Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 36:35-39 Biblia Habari Njema (BHN)

35. Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi alitawala badala yake, makao yake makuu yakiwa katika mji wa Avithi. Huyu ndiye aliyewapiga na kuwashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu.

36. Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka, alitawala badala yake.

37. Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi, ulio karibu na mto Eufrate, alitawala badala yake.

38. Shauli alipofariki, Baal-hanani, mwana wa Akbori, alitawala badala yake.

39. Baal-hanani, mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi alitawala badala yake, na jina la mji wake likiwa Pau. Mkewe Akbori alikuwa Mehetabeli, binti Matredi na mjukuu wa Mezahabu.

Kusoma sura kamili Mwanzo 36