Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 36:3-13 Biblia Habari Njema (BHN)

3. na Basemathi, binti Ishmaeli, dada yake Nebayothi.

4. Ada alimzalia Esau Elifazi, naye Basemathi akamzalia Reueli.

5. Oholibama alimzalia Yeushi, Yalamu na Kora. Hao ndio watoto wa kiume wa Esau ambao wake zake walimzalia alipokaa katika nchi ya Kanaani.

6. Kisha, Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike, watu wote wa nyumbani mwake, ng'ombe wake, wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata katika nchi ya Kanaani, akahamia mahali pengine, mbali na nduguye Yakobo.

7. Alifanya hivyo kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi hata wasiweze kuishi pamoja. Nchi waliyokaa kama wageni haikuweza kuwatosha kwa sababu ya wingi wa mifugo yao.

8. Kwa hiyo, Esau akaenda kukaa katika nchi ya milima ya Seiri. Jina lingine la Esau ni Edomu.

9. Wafuatao ni wazawa wa Esau, baba ya Waedomu katika nchi ya milima ya Seiri.

10. Watoto wa kiume wa Esau walikuwa Elifazi aliyezaliwa na Ada mkewe, na Reueli aliyezaliwa na Basemathi mke wake mwingine.

11. Watoto wa kiume wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.

12. Elifazi alikuwa na suria jina lake Timna. Huyu alimzalia mwana, jina lake Amaleki.

13. Basemathi, mkewe Esau, alimzaa Reueli. Watoto wa kiume wa Reueli walikuwa Nahathi, Zera, Shama na Miza.

Kusoma sura kamili Mwanzo 36