29. Basi, hao ndio wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,
30. Dishoni, Eseri na Dishani; kila mmoja wao akiwa mkuu wa kabila lake katika nchi ya Seiri.
31. Wafuatao ni wafalme waliotawala nchi ya Edomu, kabla mfalme yeyote hajawatawala Waisraeli:
32. Bela mwana wa Beori alitawala nchi ya Edomu akiwa na makao yake makuu katika mji wa Dinhaba.
33. Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra alitawala badala yake.