Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 36:11-27 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Watoto wa kiume wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.

12. Elifazi alikuwa na suria jina lake Timna. Huyu alimzalia mwana, jina lake Amaleki.

13. Basemathi, mkewe Esau, alimzaa Reueli. Watoto wa kiume wa Reueli walikuwa Nahathi, Zera, Shama na Miza.

14. Oholibama, binti Ana, binti Sibeoni, alimzalia Esau mumewe watoto wa kiume watatu: Yeushi, Yalamu na Kora.

15. Wafuatao ni wakuu wa makabila yaliyotokana na Esau. Elifazi, aliyekuwa mzaliwa wa kwanza wa Esau aliwazaa Temani, Omari, Sefo, Kenazi,

16. Kora, Gatamu na Amaleki, kila mmoja wao akiwa mkuu wa kabila lake. Hao wote ni watoto wa kiume wa Elifazi katika nchi ya Edomu, waliotokana na Ada, mkewe Esau.

17. Reueli, mwanawe Esau, aliwazaa Nahathi, Zera, Shama na Miza, kila mmoja wao akawa mkuu wa kabila lake. Hao wote ni watoto wa kiume wa Reueli katika nchi ya Edomu, waliotokana na Basemathi, mkewe Esau.

18. Watoto wa kiume wa Oholibama, mkewe Esau, walikuwa Yeushi, Yalamu na Kora, kila mmoja wao akiwa mkuu wa kabila lake. Hao wote ni watoto wa kiume wa Oholibama, binti Ana, mkewe Esau.

19. Basi, hao ndio wazawa wa Esau yaani Edomu, kila mmoja wao akiwa mkuu wa kabila lake.

20. Wafuatao ni wazawa wa Seiri, Mhori, na ndio wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,

21. Dishoni, Eseri na Dishani; kila mmoja wao akiwa mkuu wa kabila lake miongoni mwa Wahori wa uzawa wa Seiri, katika nchi ya Edomu.

22. Watoto wa kiume wa Lotani walikuwa Hori na Hemani; na dada yake Lotani aliitwa Timna.

23. Watoto wa kiume wa Shobali walikuwa Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.

24. Watoto wa kiume wa Sibeoni walikuwa Aya na Ana. Ana ndiye aliyeziona chemchemi za maji ya moto jangwani, alipokuwa anawachunga punda wa baba yake Sibeoni.

25. Watoto wa Ana walikuwa Dishoni na dada yake mmoja aitwaye Oholibama.

26. Watoto wa kiume wa Dishoni walikuwa Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.

27. Watoto wa kiume wa Eseri walikuwa Bilhani Zaawani na Akani.

Kusoma sura kamili Mwanzo 36