Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 32:11-14 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Nakuomba uniokoe sasa kutoka kwa ndugu yangu Esau, maana nina hofu kuwa atatushambulia na kutuua sote, akina mama pamoja na watoto.

12. Wewe uliniahidi kunitendea mema na kuwafanya wazawa wangu wawe wengi kama mchanga wa bahari ambao hauhesabiki kwa wingi wake.”

13. Basi, Yakobo akalala hapo usiku huo. Kisha akatenga sehemu ya mali yake, iwe zawadi kwa ndugu yake Esau:

14. Mbuzi majike 200 na mabeberu 20, kondoo majike 200 na madume 20,

Kusoma sura kamili Mwanzo 32