Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 31:45-51 Biblia Habari Njema (BHN)

45. Basi, Yakobo akachukua jiwe, akalisimika kama nguzo ya ukumbusho.

46. Tena Yakobo akawaambia ndugu zake, “Kusanyeni mawe.” Nao wakakusanya mawe na kufanya rundo. Kisha wakala chakula karibu na rundo hilo la mawe.

47. Labani akaliita rundo hilo Yegar-sahadutha, lakini Yakobo akaliita Galeedi.

48. Labani akasema, “Rundo hili ni ushahidi kati yako na mimi leo.” Kwa hiyo Labani akaliita Galeedi,

49. na ile nguzo akaiita Mizpa akisema, “Mwenyezi-Mungu na atulinde tuwapo mbali bila kuonana.

50. Kama ukiwatesa binti zangu, au ukioa wanawake wengine zaidi ya hawa, basi ujue kwamba hakuna aliye shahidi kati yetu ila Mungu mwenyewe.”

51. Halafu Labani akamwambia Yakobo, “Tazama rundo hili la mawe na nguzo ambayo nimeisimika kati yako nami.

Kusoma sura kamili Mwanzo 31