Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 3:11-19 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mwenyezi-Mungu akamwuliza, “Nani aliyekuambia kwamba uko uchi? Je, umekula tunda la mti nililokuamuru usile?”

12. Huyo mwanamume akajibu, “Mwanamke uliyenipa akae pamoja nami ndiye aliyenipa tunda la mti huo, nami nikala.”

13. Hapo Mwenyezi-Mungu akamwuliza huyo mwanamke, “Umefanya nini wewe?” Mwanamke akamjibu, “Nyoka alinidanganya, nami nikala.”

14. Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia nyoka,“Kwa kuwa umefanya hivyo,umelaaniwa kuliko wanyama wote wa kufugwa,na kuliko wanyama wote wa porini.Kwa tumbo lako utatambaa,na kula vumbi siku zote za maisha yako.

15. Nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke,kati ya uzawa wako na uzawa wake;yeye atakiponda kichwa chako,nawe utamwuma kisigino chake.”

16. Kisha akamwambia mwanamke,“Nitakuzidishia uchungu wa kuzaa,kwa uchungu utazaa watoto.Hata hivyo utakuwa na hamu na mumeo,naye atakutawala.”

17. Kisha akamwambia huyo mwanamume,“Kwa kuwa wewe umemsikiliza mkeo,ukala matunda ya mti ambayo nilikuamuru usile;kwa hiyo, kwa kosa lako ardhi imelaaniwa.Kwa jasho utajipatia humo riziki yako,siku zote za maisha yako.

18. Ardhi itakuzalia michongoma na magugu,nawe itakubidi kula majani ya shambani.

19. Kwa jasho lako utajipatia chakulampaka utakaporudi udongoni ulimotwaliwa;maana wewe ni mavumbi, na mavumbini utarudi.”

Kusoma sura kamili Mwanzo 3