Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 25:15-29 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi na Kedema.

16. Hao ndio watoto wa kiume wa Ishmaeli, waliokuwa asili ya makabila kumi na mawili; makazi na vijiji vyao vilijulikana kwa majina yao.

17. Ishmaeli alikuwa na umri wa miaka 137 alipofariki, akajiunga na wazee wake waliotangulia.

18. Wazawa wa Ishmaeli walikaa katika eneo lililo kati ya Hawila na Shuri, mashariki ya Misri, kuelekea Ashuru. Walikaa kwa utengano na wazawa wengine wa Abrahamu.

19. Hawa ndio wazawa wa Isaka mwana wa Abrahamu.

20. Isaka alipokuwa na umri wa miaka arubaini alimwoa Rebeka, binti Bethueli, Mwaramu wa Padan-aramu. Rebeka alikuwa dada yake Labani.

21. Rebeka alikuwa tasa, kwa hiyo Isaka akamwomba Mwenyezi-Mungu. Naye Mwenyezi-Mungu akakubali ombi lake, Rebeka akapata mimba.

22. Mimba hiyo ilikuwa ya mapacha. Watoto hao wakashindana tumboni mwake Rebeka, naye akasema, “Kama hivi ndivyo mambo yalivyo, ya nini kuishi?” Basi, akaenda kumwuliza Mwenyezi-Mungu.

23. Mwenyezi-Mungu akamwambia,“Mataifa mawili yamo tumboni mwako;makabila mawili yatakayozaliwa nawe, yatafarakana.Moja litakuwa lenye nguvu kuliko lingine;mkubwa atamtumikia mdogo.”

24. Siku zake za kujifungua zilipotimia, Rebeka alijifungua mapacha.

25. Wa kwanza alikuwa mwekundu, mwenye nywele mwili wote; hivyo wakamwita Esau.

26. Wa pili alizaliwa akiwa amemshika Esau kisigino, hivyo wakampa jina Yakobo. Isaka alikuwa na umri wa miaka sitini wakati Esau na Yakobo walipozaliwa.

27. Watoto hao wakakua; Esau akawa mwindaji hodari, mpenda maisha ya mbugani, na Yakobo akawa mtu mtulivu, mpenda maisha ya nyumbani.

28. Basi, Isaka akampenda Esau kwa sababu alipenda kula mawindo yake, lakini Rebeka akampenda Yakobo.

29. Siku moja, Yakobo alipokuwa anapika dengu, Esau alirudi nyumbani kutoka mawindoni ana njaa sana.

Kusoma sura kamili Mwanzo 25