Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 25:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Abrahamu alioa mke mwingine, jina lake Ketura.

2. Ketura alimzalia Abrahamu: Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua.

3. Yokshani alimzaa Sheba na Dedani; wazawa wa Dedani walikuwa Waashuru, Waletushi na Waleumi.

4. Watoto wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Henoki, Abida na Eldaa. Wote hao walikuwa wazawa wa Ketura.

5. Abrahamu alimrithisha Isaka mali yake yote.

6. Lakini watoto wa kiume wa masuria wake akawapa zawadi, na wakati alipokuwa bado hai, aliwapeleka katika nchi ya mashariki, mbali na Isaka mwanawe.

7. Abrahamu aliishi miaka 175.

8. Alifariki baada ya kuishi maisha marefu na ya fanaka, akajiunga na wazee wake waliomtangulia.

Kusoma sura kamili Mwanzo 25