25. Kwetu kuna majani na malisho ya kutosha na mahali pa kulala wageni.”
26. Ndipo yule mtu akainamisha kichwa chake, akamwabudu Mwenyezi-Mungu
27. akisema, “Atukuzwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hajasahau fadhili zake na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mwenyezi-Mungu ameniongoza mimi mwenyewe moja kwa moja hadi kwa jamaa ya bwana wangu!”
28. Kisha yule msichana akakimbia kwenda kuwapa habari jamaa za mama yake.
29. Rebeka alikuwa na kaka yake aitwaye Labani. Labani akatoka mbio kukutana na yule mtu kisimani.