Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 24:25-29 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Kwetu kuna majani na malisho ya kutosha na mahali pa kulala wageni.”

26. Ndipo yule mtu akainamisha kichwa chake, akamwabudu Mwenyezi-Mungu

27. akisema, “Atukuzwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hajasahau fadhili zake na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mwenyezi-Mungu ameniongoza mimi mwenyewe moja kwa moja hadi kwa jamaa ya bwana wangu!”

28. Kisha yule msichana akakimbia kwenda kuwapa habari jamaa za mama yake.

29. Rebeka alikuwa na kaka yake aitwaye Labani. Labani akatoka mbio kukutana na yule mtu kisimani.

Kusoma sura kamili Mwanzo 24