Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 22:10-15 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Abrahamu akaunyosha mkono wake, akatwaa kisu tayari kumchinja mwanawe.

11. Lakini malaika wa Mwenyezi-Mungu akamwita kutoka mbinguni, “Abrahamu! Abrahamu!” Naye akaitika, “Naam, nasikiliza!”

12. Malaika akamwambia, “Usimdhuru mtoto wala usimfanye lolote! Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwani hukuninyima hata mwanao wa pekee.”

13. Ndipo Abrahamu akatazama, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake kichakani. Basi, akaenda, akamchukua huyo kondoo, akamtoa sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.

14. Kwa hiyo, Abrahamu akapaita mahali hapo, “Mwenyezi-Mungu hujalia.” Kama isemwavyo hata leo, “Katika mlima wa Mwenyezi-Mungu, watu hujaliwa.”

15. Malaika wa Mwenyezi-Mungu akamwita Abrahamu mara ya pili kutoka mbinguni,

Kusoma sura kamili Mwanzo 22