Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 2:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Hivyo ndivyo mbingu na dunia zilivyokamilika pamoja na vitu vyote vilivyomo.

2. Siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyofanya; siku hiyo ya saba Mungu akapumzika baada ya kazi yake yote aliyofanya.

3. Mungu akaibariki siku ya saba na kuitakasa, kwa kuwa siku hiyo Mungu alipumzika baada ya kazi yake yote ya kuumba.

4. Hivyo ndivyo mbingu na dunia zilivyoumbwa.Siku ile Mwenyezi-Mungu alipoziumba mbingu na dunia,

5. Hapakuwa na mimea juu ya nchi wala miti haikuwa imechipua kwani Mwenyezi-Mungu hakuwa ameinyeshea nchi mvua, wala hapakuwa na mtu wa kuilima.

6. Hata hivyo, maji yalitoka ardhini yakainywesha ardhi yote.

7. Basi, Mwenyezi-Mungu akamfanya mwanamume kwa mavumbi ya udongo, akampulizia puani pumzi ya uhai, na huyo mwanamume akawa kiumbe hai.

Kusoma sura kamili Mwanzo 2