Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 11:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kwanza, watu wote duniani walikuwa na lugha moja na walitumia maneno yaleyale.

2. Basi, ikawa watu waliposafirisafiri kutoka mashariki, walifika katika nchi tambarare huko Shinari, wakakaa.

3. Kisha wakaambiana, “Haya! Na tufyatue matofali, tuyachome moto vizuri.” Walikuwa na matofali badala ya mawe, na lami badala ya chokaa.

4. Wakasema, “Na tujijengee mji na mnara ambao kilele chake kitafika mbinguni ili tujipatie jina, tusije tukatawanyika duniani kote.”

5. Ndipo Mwenyezi-Mungu akashuka chini kuuona mji huo na mnara walioujenga binadamu.

6. Mwenyezi-Mungu akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na wote wana lugha moja; huu ni mwanzo tu wa yale watakayoyafanya. Lolote wanalokusudia kulifanya watafanikiwa.

7. Haya, na tushuke chini na kuivuruga lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”

Kusoma sura kamili Mwanzo 11