Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 1:14-21 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Mungu akasema, “Mianga na iweko angani, itenge mchana na usiku, ioneshe nyakati, majira, siku na miaka,

15. na ingae angani na kuiangazia dunia.” Ikawa hivyo.

16. Basi, Mungu akafanya mianga miwili mikubwa; ule mkubwa utawale mchana na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia.

17. Mungu akaiweka mianga hiyo angani iiangazie dunia,

18. ipate kutawala mchana na usiku, na kuutenga mwanga na giza. Mungu akaona kuwa ni vyema.

19. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya nne.

20. Mungu akasema, “Maji na yatoe makundi ya viumbe hai na ndege waruke angani.”

21. Basi, Mungu akaumba wanyama wakubwa sana wa baharini na aina zote za viumbe vyote hai viendavyo na kujaa majini; akaumba na aina zote za ndege wote. Mungu akaona kuwa ni vyema.

Kusoma sura kamili Mwanzo 1