Agano la Kale

Agano Jipya

Mwanzo 1:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia.

2. Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho ya Mungu ilikuwa ikitanda juu ya maji.

3. Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa.

4. Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza,

5. mwanga akauita “Mchana” na giza akaliita “Usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya kwanza.

Kusoma sura kamili Mwanzo 1