Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 7:16-20 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Nao watu wa mataifa watakapoona hayo,watajaa fedheha hata kama wana nguvu.Watashikwa na bumbuazi na kukosa cha kusemana kuwa kama viziwi.

17. Watatambaa mavumbini kama nyoka;naam, kama viumbe watambaao.Watatoka katika ngome zaohuku wanatetemeka na kujaa hofu.Watakugeukia wewe Mungu wetu kwa hofu,wataogopa kwa sababu yako.

18. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?Wewe wasamehe dhambi za watu wako waliobaki,wala huyaangalii makosa yao.Hasira yako haidumu milele,ila wapendelea zaidi kutuonesha fadhili zako.

19. Utatuhurumia tena, ee Mwenyezi-Mungu;utafutilia mbali dhambi zetu,utazitupa zote katika vilindi vya bahari.

20. Utaonesha uaminifu wako na rehema zakokwa wazawa wa Abrahamu na wa Yakobo,kama ulivyowaahidi wazee wetu tangu zamani.

Kusoma sura kamili Mika 7