Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 7:13-20 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Lakini nchi yote nyingine itakuwa jangwa,kwa sababu ya uovu wa wakazi wake.

14. Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako,uwachunge hao walio kundi lako mwenyeweambao wanaishi peke yao katika msituwamezungukwa na ardhi yenye rutuba.Uwachunge kama ulivyofanya pale awalikatika malisho ya Bashani na Gileadi.

15. Kama wakati ulipotutoa nchini Misri,utuoneshe tena maajabu yako.

16. Nao watu wa mataifa watakapoona hayo,watajaa fedheha hata kama wana nguvu.Watashikwa na bumbuazi na kukosa cha kusemana kuwa kama viziwi.

17. Watatambaa mavumbini kama nyoka;naam, kama viumbe watambaao.Watatoka katika ngome zaohuku wanatetemeka na kujaa hofu.Watakugeukia wewe Mungu wetu kwa hofu,wataogopa kwa sababu yako.

18. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?Wewe wasamehe dhambi za watu wako waliobaki,wala huyaangalii makosa yao.Hasira yako haidumu milele,ila wapendelea zaidi kutuonesha fadhili zako.

19. Utatuhurumia tena, ee Mwenyezi-Mungu;utafutilia mbali dhambi zetu,utazitupa zote katika vilindi vya bahari.

20. Utaonesha uaminifu wako na rehema zakokwa wazawa wa Abrahamu na wa Yakobo,kama ulivyowaahidi wazee wetu tangu zamani.

Kusoma sura kamili Mika 7