Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 6:5-8 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Enyi watu wangu,kumbukeni njama za Balaki mfalme wa Moabu,na jinsi Balaamu mwana wa Beori alivyomjibu.Kumbukeni yaliyotukia njiani kati ya Shitimu na Gilgali.Kumbukeni mtambue matendo yangu ya kuwaokoa!”

6. Nimwendee Mwenyezi-Mungu na kitu gani,nipate kumwabudu Mungu aliye juu?Je, nimwendee na sadaka za kuteketezwa,nimtolee ndama wa mwaka mmoja?

7. Je, Mwenyezi-Mungu atapendezwanikimtolea maelfu ya kondoo madume,au mito elfu na elfu ya mafuta?Je, nimtolee mzaliwa wangu wa kwanzakwa ajili ya kosa langu,naam, mtoto wangukwa ajili ya dhambi yangu?

8. Mungu amekuonesha yaliyo mema, ewe mtu;anachotaka Mwenyezi-Mungu kwako ni hiki:Kutenda mambo ya haki,kupenda kuwa na huruma,na kuishi kwa unyenyekevu na Mungu wako.

Kusoma sura kamili Mika 6