Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 6:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Sikilizeni anachosema Mwenyezi-Mungu:“Wewe nabii, nenda ukailalamikie milima,navyo vilima visikie sauti yako.”

2. Sikilizeni kesi ya Mwenyezi-Mungu enyi milima,sikilizeni enyi misingi ya kudumu ya dunia!Mwenyezi-Mungu anayo kesi dhidi ya watu wake.Yeye atatoa mashtaka dhidi ya Waisraeli.

3. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Enyi watu wangu, nimewatendea nini?Nimewachosha kwa kitu gani?Nijibuni!

4. Mimi niliwatoa nchini Misri;niliwakomboa kutoka utumwani;niliwapeni Mose, Aroni na Miriamu kuwaongoza.

5. Enyi watu wangu,kumbukeni njama za Balaki mfalme wa Moabu,na jinsi Balaamu mwana wa Beori alivyomjibu.Kumbukeni yaliyotukia njiani kati ya Shitimu na Gilgali.Kumbukeni mtambue matendo yangu ya kuwaokoa!”

6. Nimwendee Mwenyezi-Mungu na kitu gani,nipate kumwabudu Mungu aliye juu?Je, nimwendee na sadaka za kuteketezwa,nimtolee ndama wa mwaka mmoja?

7. Je, Mwenyezi-Mungu atapendezwanikimtolea maelfu ya kondoo madume,au mito elfu na elfu ya mafuta?Je, nimtolee mzaliwa wangu wa kwanzakwa ajili ya kosa langu,naam, mtoto wangukwa ajili ya dhambi yangu?

8. Mungu amekuonesha yaliyo mema, ewe mtu;anachotaka Mwenyezi-Mungu kwako ni hiki:Kutenda mambo ya haki,kupenda kuwa na huruma,na kuishi kwa unyenyekevu na Mungu wako.

9. Mwenyezi-Mungu anawaita wakazi wa mji,na ni jambo la busara sana kumcha yeye:“Sikilizeni, enyi watu wa Yuda;sikilizeni enyi mliokusanyika mjini.

Kusoma sura kamili Mika 6