Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 4:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mataifa mengine hufuata njia zao,kwa kuitegemea miungu yao,lakini sisi twafuata njia zetu kwa kumtegemea Mwenyezi-Mungu,Mungu wetu, milele na milele.

6. Mwenyezi-Mungu asema,“Siku ile nitawakusanya walemavu,naam, nitawakusanya waliochukuliwa uhamishoni,watu wale ambao niliwaadhibu.

7. Hao walemavu ndio watakaobaki hai;hao waliochukuliwa uhamishoni watakuwa taifa lenye nguvu.Nami Mwenyezi-Mungu nitawatawala mlimani Siyoni,tangu wakati huo na hata milele.”

8. Nawe kilima cha Yerusalemu,wewe ngome ya Siyoni,ambamo Mungu anafanya ulinzi juu ya watu wake,kama mchungaji juu ya kondoo wake;wewe utakuwa tena mji maarufu kama hapo awali,Yerusalemu utakuwa tena mji mkuu wa mfalme.

9. Sasa kwa nini mnalia kwa sauti?Je, hamna mfalme tena?Mshauri wenu ametoweka?Mnapaza sauti ya uchungu,kama mama anayejifungua!

Kusoma sura kamili Mika 4