Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 4:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Utakuja wakati ambapomlima wa nyumba ya Mwenyezi-Munguutakuwa mkubwa kuliko milima yote.Naam, utakwezwa juu ya vilima vyote.Watu wengi watamiminika huko,

2. mataifa mengi yataujia na kusema:“Twendeni juu kwenye mlima wa Mwenyezi-Mungu,twende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo,ili atufundishe njia zake,nasi tufuate nyayo zake.Maana mwongozo utatoka huko Siyoni;neno la Mwenyezi-Mungu huko Yerusalemu.”

3. Mungu atasuluhisha mizozo ya mataifa mengi,atakata mashauri ya mataifa makubwa ya mbali.Nayo yatafua mapanga yao kuwa majembe,na mikuki yao kuwa miundu ya kupogolea.Taifa halitapigana na taifa lingine,wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.

Kusoma sura kamili Mika 4