Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 3:9-12 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Sikieni jambo hili enyi viongozi wa wazawa wa Yakobo,sikilizeni, enyi watawala wa Waisraeli:Nyinyi mnachukia mambo ya hakina kupotosha mambo ya adili.

10. Nyinyi mnajenga mji wa Siyoni kwa damu,naam, mji wa Yerusalemu kwa dhuluma.

11. Waamuzi hufanya kazi yao kwa rushwa,makuhani wake hufundisha kwa malipo,manabii hutabiri kwa fedha.Hata hivyo hujidai kumtegemea Mwenyezi-Mungu,wakisema, “Mwenyezi-Mungu, si yupo pamoja nasi?Hatutapatwa na madhara yoyote!”

12. Haya! Kwa sababu yenu,Siyoni utalimwa kama shamba,Yerusalemu utakuwa magofu,nao mlima wa hekalu utakuwa msitu.

Kusoma sura kamili Mika 3