Agano la Kale

Agano Jipya

Mika 3:6-9 Biblia Habari Njema (BHN)

6. “Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono,kutakuwa giza kwenu bila ufunuo.Kwenu manabii kutakuchwa,mchana utakuwa giza kwenu.”

7. Mabingwa wa maono watafedheheka,mafundi wa kubashiri wataaibishwa;wote watafunga midomo yao,maana hawatapata jibu lolote kutoka kwa Mungu.

8. Lakini kwa upande wangu,nimejazwa nguvu na roho ya Mwenyezi-Mungu;nimejaliwa kujua haki na kuwa na uwezoniwatangazie wazawa wa Yakobo kosa lao,niwaambie Waisraeli dhambi yao.

9. Sikieni jambo hili enyi viongozi wa wazawa wa Yakobo,sikilizeni, enyi watawala wa Waisraeli:Nyinyi mnachukia mambo ya hakina kupotosha mambo ya adili.

Kusoma sura kamili Mika 3