6. “Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono,kutakuwa giza kwenu bila ufunuo.Kwenu manabii kutakuchwa,mchana utakuwa giza kwenu.”
7. Mabingwa wa maono watafedheheka,mafundi wa kubashiri wataaibishwa;wote watafunga midomo yao,maana hawatapata jibu lolote kutoka kwa Mungu.
8. Lakini kwa upande wangu,nimejazwa nguvu na roho ya Mwenyezi-Mungu;nimejaliwa kujua haki na kuwa na uwezoniwatangazie wazawa wa Yakobo kosa lao,niwaambie Waisraeli dhambi yao.
9. Sikieni jambo hili enyi viongozi wa wazawa wa Yakobo,sikilizeni, enyi watawala wa Waisraeli:Nyinyi mnachukia mambo ya hakina kupotosha mambo ya adili.