Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 9:15-18 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Katika mji huo, alikuwapo maskini mmoja mwenye hekima, ambaye, kwa hekima yake aliuokoa mji huo. Lakini hakuna mtu aliyemkumbuka huyo maskini baadaye.

16. Basi, mimi nasema, hekima ni bora kuliko nguvu, ingawa hekima ya maskini haithaminiwi, na maneno yake hayasikilizwi.

17. Afadhali kusikiliza maneno matulivu ya mwenye hekima,kuliko kusikiliza kelele za mfalme katika kikao cha wapumbavu.

18. Kuwa na hekima ni bora kuliko kutegemea silaha,lakini mwenye dhambi mmoja huharibu mazuri mengi.

Kusoma sura kamili Mhubiri 9