Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 4:13-16 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Afadhali kijana maskini mwenye hekima kuliko mfalme mzee mpumbavu, ambaye hasikilizi shauri jema;

14. hata ikiwa alikuwa mfungwa na sasa ni mfalme, au alizaliwa maskini na sasa ni mfalme.

15. Niliwaona watu wote waishio duniani, hata yule kijana ambaye angechukua nafasi ya mfalme.

16. Idadi ya watu haikuwa na kikomo, naye aliwatawala wote. Hata hivyo, wale wanaozaliwa baadaye hawatamfurahia. Hakika hayo nayo ni bure kabisa na kufukuza upepo.

Kusoma sura kamili Mhubiri 4