Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 3:7-12 Biblia Habari Njema (BHN)

7. wakati wa kurarua na wakati wa kushona;wakati wa kukaa kimya na wakati wa kuongea;

8. wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia;wakati wa vita na wakati wa amani.

9. Mfanyakazi hufaidi nini kutokana na juhudi zake hizo?

10. Mimi nimeiona kazi ambayo binadamu amepewa na Mungu.

11. Mungu amekifanya kila kitu kiwe kizuri kwa wakati wake. Amempa binadamu hamu ya kujua mambo ya baadaye, lakini hajamjalia fursa ya kuelewa matendo yake Mungu tangu mwanzo mpaka mwisho.

12. Najua kwamba, kwa binadamu, liko jambo moja tu la kumfaa; kufurahi na kujifurahisha muda wote aishipo.

Kusoma sura kamili Mhubiri 3