2. Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa;wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa;
3. wakati wa kuua na wakati wa kuponya;wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga;
4. wakati wa kulia na wakati wa kucheka;wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza;
5. wakati wa kutupa mawe na wakati wa kuyakusanya mawe pamoja;wakati wa kukumbatia na wakati wa kuacha kukumbatia;
6. wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza;wakati wa kuhifadhi na wakati wa kutupa;
7. wakati wa kurarua na wakati wa kushona;wakati wa kukaa kimya na wakati wa kuongea;
8. wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia;wakati wa vita na wakati wa amani.
9. Mfanyakazi hufaidi nini kutokana na juhudi zake hizo?
10. Mimi nimeiona kazi ambayo binadamu amepewa na Mungu.