Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 3:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kila kitu kina majira yake,kila jambo duniani lina wakati wake:

2. Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa;wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa;

3. wakati wa kuua na wakati wa kuponya;wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga;

4. wakati wa kulia na wakati wa kucheka;wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza;

5. wakati wa kutupa mawe na wakati wa kuyakusanya mawe pamoja;wakati wa kukumbatia na wakati wa kuacha kukumbatia;

6. wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza;wakati wa kuhifadhi na wakati wa kutupa;

7. wakati wa kurarua na wakati wa kushona;wakati wa kukaa kimya na wakati wa kuongea;

8. wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia;wakati wa vita na wakati wa amani.

Kusoma sura kamili Mhubiri 3