1. Kila kitu kina majira yake,kila jambo duniani lina wakati wake:
2. Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa;wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa;
3. wakati wa kuua na wakati wa kuponya;wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga;
4. wakati wa kulia na wakati wa kucheka;wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza;
5. wakati wa kutupa mawe na wakati wa kuyakusanya mawe pamoja;wakati wa kukumbatia na wakati wa kuacha kukumbatia;