Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 2:2-6 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Nikasema kuhusu kicheko, “Ni wazimu”, na starehe “Mna faida gani?”

3. Nilifikiria sana, namna ya kujichangamsha akili kwa divai, huku nikisukumwa na ari yangu ya kupata hekima; pia namna ya kuandamana na upumbavu ili nione yaliyo bora kabisa ambayo wanadamu wanaweza wakafanya waishipo maisha yao mafupi hapa duniani.

4. Nilifanya mambo makuu: Nilijenga majumba na kujilimia mashamba ya mizabibu.

5. Nilijifanyia bustani na viunga, nikapanda miti ya matunda ya kila aina.

6. Nilijichimbia mabwawa ya maji ya kumwagilia hiyo miti.

Kusoma sura kamili Mhubiri 2