2. Nikasema kuhusu kicheko, “Ni wazimu”, na starehe “Mna faida gani?”
3. Nilifikiria sana, namna ya kujichangamsha akili kwa divai, huku nikisukumwa na ari yangu ya kupata hekima; pia namna ya kuandamana na upumbavu ili nione yaliyo bora kabisa ambayo wanadamu wanaweza wakafanya waishipo maisha yao mafupi hapa duniani.
4. Nilifanya mambo makuu: Nilijenga majumba na kujilimia mashamba ya mizabibu.
5. Nilijifanyia bustani na viunga, nikapanda miti ya matunda ya kila aina.
6. Nilijichimbia mabwawa ya maji ya kumwagilia hiyo miti.