Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 2:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Basi, nikawaza; “Ngoja nijitumbukize katika starehe, nijifurahishe.” Lakini, niligundua kwamba kufanya hivyo ni bure kabisa.

2. Nikasema kuhusu kicheko, “Ni wazimu”, na starehe “Mna faida gani?”

3. Nilifikiria sana, namna ya kujichangamsha akili kwa divai, huku nikisukumwa na ari yangu ya kupata hekima; pia namna ya kuandamana na upumbavu ili nione yaliyo bora kabisa ambayo wanadamu wanaweza wakafanya waishipo maisha yao mafupi hapa duniani.

4. Nilifanya mambo makuu: Nilijenga majumba na kujilimia mashamba ya mizabibu.

5. Nilijifanyia bustani na viunga, nikapanda miti ya matunda ya kila aina.

6. Nilijichimbia mabwawa ya maji ya kumwagilia hiyo miti.

7. Nilinunua watumwa, wanawake kwa wanaume, na wengine wakazaliwa nyumbani mwangu. Nilikuwa na mali nyingi, makundi ya ng'ombe na kondoo wengi kuliko mtu yeyote aliyenitangulia kukaa Yerusalemu.

8. Nilijirundikia fedha na dhahabu kutoka hazina za wafalme na toka mikoani, nami nilipata waimbaji wanaume kwa wanawake, na masuria watamaniwao.

Kusoma sura kamili Mhubiri 2