Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 2:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Basi, nikawaza; “Ngoja nijitumbukize katika starehe, nijifurahishe.” Lakini, niligundua kwamba kufanya hivyo ni bure kabisa.

2. Nikasema kuhusu kicheko, “Ni wazimu”, na starehe “Mna faida gani?”

3. Nilifikiria sana, namna ya kujichangamsha akili kwa divai, huku nikisukumwa na ari yangu ya kupata hekima; pia namna ya kuandamana na upumbavu ili nione yaliyo bora kabisa ambayo wanadamu wanaweza wakafanya waishipo maisha yao mafupi hapa duniani.

Kusoma sura kamili Mhubiri 2