Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 10:10-15 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Nguvu nyingi zaidi zahitajikakwa mtumiaji shoka butu lisilonolewa,lakini kutumia hekima humfanya mtu afanikiwe.

11. Nyoka akiuma kabla hajachochewa,mchochezi hahitajiki tena.

12. Maneno ya mwenye hekima humnufaisha asemaye;lakini midomo ya mpumbavu humwangamiza.

13. Mpumbavu huanza kusema kwa maneno ya kijinga,na kumaliza kauli yake kwa wazimu mbaya.

14. Mpumbavu hububujika maneno.Binadamu hajui yatakayokuwako,wala yale yatakayotukia baada yake.

15. Mpumbavu huchoshwa na kazi yakehata asijue njia ya kurudia nyumbani.

Kusoma sura kamili Mhubiri 10