Agano la Kale

Agano Jipya

Mhubiri 10:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nzi waliokufa husababisha marashi kunuka;upumbavu kidogo hubatilisha hekima na heshima.

2. Moyo wa mwenye hekima humwongoza kutenda yaliyo sawa;lakini mtu mpumbavu moyo wake humpotosha.

3. Hata apitapo njiani, mpumbavu hutambulikana hivyo,humjulisha kila mtu kwamba yeye ni mpumbavu.

4. Mtawala akikuwakia hasira, usijiuzulu;makosa makubwa huweza kufutwa ukiwa mnyenyekevu.

5. Kuna uovu niliogundua hapa duniani, uovu unaosababishwa na watawala:

6. Kwamba wapumbavu wanapewa kazi za madaraka ya juu, na matajiri wanachukua nafasi za mwisho.

7. Nimeona watumwa wanapanda farasi, na wakuu wanatembea kwa miguu kama watumwa.

Kusoma sura kamili Mhubiri 10