1. Nzi waliokufa husababisha marashi kunuka;upumbavu kidogo hubatilisha hekima na heshima.
2. Moyo wa mwenye hekima humwongoza kutenda yaliyo sawa;lakini mtu mpumbavu moyo wake humpotosha.
3. Hata apitapo njiani, mpumbavu hutambulikana hivyo,humjulisha kila mtu kwamba yeye ni mpumbavu.
4. Mtawala akikuwakia hasira, usijiuzulu;makosa makubwa huweza kufutwa ukiwa mnyenyekevu.