Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 7:8-13 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Huyo alikuwa akitembea kwenye barabara ile,karibu na kona alikoishi mwanamke fulani.Basi akashika njia iendayo nyumbani kwa mwanamke huyo.

9. Ilikuwa yapata wakati wa jioni,giza na usiku vilikuwa vimeanza kuingia.

10. Punde kijana akakutana na huyo mwanamke;amevalia kama malaya, ana mipango yake.

11. Alikuwa mwanamke wa makelele na mkaidi;miguu yake haitulii nyumbani:

12. Mara barabarani, mara sokoni,katika kila kona ya njia hakosekani akivizia.

13. Alimkumbatia kijana huyo na kumbusu,na kwa maneno matamu, akamwambia:

Kusoma sura kamili Methali 7