Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 7:6-20 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Siku moja dirishani mwa nyumba yangu,nilichungulia nje kupitia viunzi vya dirisha,

7. nikawaona vijana wengi wajinga,na mmoja hasa aliyekuwa mpumbavu.

8. Huyo alikuwa akitembea kwenye barabara ile,karibu na kona alikoishi mwanamke fulani.Basi akashika njia iendayo nyumbani kwa mwanamke huyo.

9. Ilikuwa yapata wakati wa jioni,giza na usiku vilikuwa vimeanza kuingia.

10. Punde kijana akakutana na huyo mwanamke;amevalia kama malaya, ana mipango yake.

11. Alikuwa mwanamke wa makelele na mkaidi;miguu yake haitulii nyumbani:

12. Mara barabarani, mara sokoni,katika kila kona ya njia hakosekani akivizia.

13. Alimkumbatia kijana huyo na kumbusu,na kwa maneno matamu, akamwambia:

14. “Ilinilazimu kutoa tambiko zangu;leo hii nimekamilisha nadhiri yangu.

15. Ndio maana nimetoka ili nikulaki,nimekutafuta kwa hamu nikakupata.

16. Nimetandika kitanda changu vizuri,kwa shuka za rangi za kitani kutoka Misri.

17. Nimekitia manukato, manemane, udi na mdalasini.

18. Njoo tulale pamoja mpaka asubuhi;njoo tujifurahishe kwa mahaba.

19. Mume wangu hayumo nyumbani,amekwenda safari ya mbali.

20. Amechukua bunda la fedha;hatarejea nyumbani karibuni.”

Kusoma sura kamili Methali 7