Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 31:16-20 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Hufikiria kununua shamba, kisha hulinunua,na kulima zabibu kwa faida ya jasho lake.

17. Huwa tayari kufanya kazi kwa nguvuna kuiimarisha mikono yake.

18. Hutambua kwamba shughuli zake zina faida;hufanya kazi hata usiku kwa mwanga wa taa yake.

19. Husokota nyuzi kwa mikono yake mwenyewe,kwa vidole vyake mwenyewe husuka nguo zake.

20. Huufungua mkono wake kuwapa maskini,hunyosha mkono kuwasaidia fukara.

Kusoma sura kamili Methali 31