Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 31:13-18 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Hutafuta sufu na kitani,na kufanya kazi kwa mikono yake kwa bidii.

14. Yeye ni kama meli za biashara:Huleta chakula chake kutoka mbali.

15. Huamka kabla ya mapambazuko,akaitayarishia jamaa yake chakula,na kuwagawia kazi watumishi wake.

16. Hufikiria kununua shamba, kisha hulinunua,na kulima zabibu kwa faida ya jasho lake.

17. Huwa tayari kufanya kazi kwa nguvuna kuiimarisha mikono yake.

18. Hutambua kwamba shughuli zake zina faida;hufanya kazi hata usiku kwa mwanga wa taa yake.

Kusoma sura kamili Methali 31